PEACE CLUB


NINI MAANA NA CHIMBUKO LA TPIF

Tanzania Peace Initiative Foundation ni asasi ya kiraia iliyo sajiliwa kisheria kwa upande wa Tanzania bara asasi hiyi ili sajiliwa chini ya kifungu cha 12(2) Act No 24 ya mwaka 2002, na Namba yake ya usajili ni 00NGO/00006106. Kwa upande wa Zanzibar asasi hii ilisajiliwa kwa sheria namba 6 ya mwaka 1995.

Asasi hii imeanzishwa kutokana na hali ya amani ya nchi ya Tanzania kuonekana kuwa ustawi wake unazorota, tathmini hii ilifanyika kwa kuwashirikisha wadau mbali mbali wenye uelewa katika maswala ya amani ya nchi hasa wale walio somea maswala ya husuyo utatuzi wa migogoro na ujengaji wa amani, wanasiasa wakongwe na wazee wanao ijuwa historia ya Tanzania tangu ipate uhuru wake mwaka 1961.

Ustawi wa amani huendana na maendeleo ya kisiasa kiuchumi na kijamii; ustawi wa amani hubeba dhana ya kurithishwa; tena machafuko ni adui wa hayo yote na zaidi sana huwaathiri watoto na wanawake.

Kutokana na uchunguzi huo wa kina uliowahusisha wataalam wa maswaala ya utatuzi wa migogoro na ujenzi wa amani wenye ueledi,  TPIF ilibidi  kuzaliwa na kusajiliwa kisheria ili kuweza kuiarifu jamii kwa kutoa elimu na kuisemea amani kuhusu ustawi wake nchini.

MALENGO YA TPIF kwa ufupi

MALENGO/MADHUMUNI

1.      Kuelimisha na kuongeza uelewa juu ya umuhimu wa amani na maendeleo kwa jamii

2.       Kurahisisha ujenzi wa amani kwa kushajihisha haki za binaadamu na demokrasiya.

3.      Kurahisisha utatuzi wa migogoro na kuidhibiti katika jamii, taifa na kimataifa.

 

DHANA YA VIKUNDI VYA AMANI

Moja kati ya mbinu ama njia iliyo ridhiwa kuwekwa kwenye kutimiza azima ya TPIF kuisemea amani ni kufungua vikundi vya amani ambavyo vitatumika kama vyombo vitakavyo isemea amani ya Tanzania kwa kuigusa jamii kwa ukaribu zaidi ili kukuza ustawi wa amani yetu kwa ujumla.

Vikundi hivi vya amani vitafunguliwa kwenye mikoa ya nchi nzima ya Tanzania ambapo mpango huu utatekelezwa kwa awamu ukianza na Zanzibar,  Dar-Es-Salaam, Mwanza, Tabora, Morogoro, Pwani, Arusha, na Mtwara

Masharti ya pamoja ya kujiunga na vikundi vya amani

 Mtu yeyote alie ni mtanzania, mzalendo tena mpenda amani anaweza kujiunga na VIKUNDI VYA AMANI kama mtu wa kujitolea bila ya pingamizi bali tu awe amekidhi vigezo vilivyo ainishwa kwenye kipengele hiki. Na niutaratibu kuwa ili mtu awe mwanachama au mtu wa kujitolea (Volunteer) halisi basi mtu huyo imempasa ajaze fomu nakupitiwa na uongozi wa TPIF ili kuungwa kuwa kama alivyo kusudia mwenyewe. Taasisi hii haita athiri muda wa kujitafutia maendeleo kwa mtu yeyote atakae jitolea bali kwa ridhaa yake, utashi, na uzalendo wake mwenyewe.

FAIDA ZA KUJIUNGA NA vikundi vya amani

1.         Mwanachama yeyote atakae jiunga na vikundi vya amani atapata fursa ya kuhudhuria makongamano, seminars na workshorp mbali mbali zitakazo endeshwa na TPIF ama asasi yeyote ya kiraia yenye uhusiano na TPIF.

2.       Mwanachama atapata kuunganishwa na vikundi vya wajasiriamali wazoefu; mabenki yenye mikopo ya riba nafuu; na wizara zenye mipango na Vijana kwa kundi la Vijana. Ijapokua lika la mtu halitoathiri fursa ya mtu yeyote katika kutimiza azma ya amani na maendeleo.

3.       Mwanachama atapata haki ya kulipwa katika kila semina, kongamano, au workshop yeyote itakayo endeshwa kwa malipo.

4.        Mwanachama atatapata fursa ya kutembea ndani na nje ya nchi ili kuzidi kujifunza.

SERA YA UTEKELEZAJI MAJUKUMU

Asasi hii inazingatia kua, kila mtu atatekeleza wajibu wake bila ya kuvunja sheria za nchi wala taratibu zozote zilizowekwa kisheria. Tena shughuli za vikundi hivyo havitatakiwa kuharibu shughuli binafsi za mwanachama katika utekelezaji wake wa majukumu.

Washiriki

1.         Kituo cha utafiti na utatuzi wa migogoro cha Africa

 

IMAMU M. VUAI

TPIF EXECUTIVE SECRETARY

 

No comments: